TAARIFA KWA UMMA
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania inautaarifu umma kuwa utaratibu wa
kuomba udahili kwa vyuo vya elimu ya juu ambavyo bado vina nafasi
unaandaliwa na kwa mantiki hiyo wale wote ambao hawana udahili kwa
sasa na wangependa kuomba kujiunga na vyuo hivyo katika mwaka wa
masomo 2011/12 wasubiri mpaka utaratibu huo utakapotangazwa na
Tume kuanzia tarehe 26 Septemba 2011.
Matangazo ambayo yametolewa na Chuo Kikuu cha Dar es salaam
kuitisha udahili zaidi kwa sababu ya chuo hicho kuwa na nafasi katika
programu mbalimbali ni ishara kwamba bado kuna nafasi katika programu
za chuo hicho na hivyo wanafunzi wasubiri utaratibu wa kuomba udahili
katika vyuo utakapotangazwa na Tume kuanzia tarehe 26 Septemba 2011
ili kuepuka usumbufu wanaoweza kuupata hapo baadaye.
Kwa taarifa hii vyuo vikuu vyote nchini vinataarifiwa kusubiri utaratibu
utakapotangazwa kabla ya kutoa matangazo yao. Pia vyuo vyote vya
elimu ya juu ambavyo bado vina nafasi kwa ajili ya wanafunzi kwa
mwaka wa masomo wa 2011/12 vinataarifiwa kutuma taarifa hizo kwa
Tume ili programu husika ziweze kuongezwa kwenye mfumo kabla ya
tarehe 26 Septemba 2011.
Heri ya miaka 50 ya Uhuru
Katibu Mtendaji
TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA
No comments:
Post a Comment